Sat, 14 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Manchester United Erik Ten Hag amethibitisha kuwa kiungo wake Donny Van De Beek atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi chote cha msimu huu kutokana na kukumbwa na majeraha.
Mara ya mwisho kwa mchezaji huyo kuonekana uwanjani ni katika ushindi dhidi ya Bournemouth Januari 3 na alitolewa mapema mwishoni mwa kipindi cha kwanza baada ya kufanyiwa faulo.
Na sasa taarifa kamili zimethibitisha kuwa itamchukua muda kupona hivyo hatoweza kurudi Uwanjani kwa msimu huu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live