Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyota Dodoma Jiji awatisha Simba

Mkandala Dom Wachezaji wa Dodoma wakishangilia goli dhidi ya Ruvu Shooting

Thu, 30 Sep 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchezaji wa Dodoma Jiji, Cleophance Mkandala ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba ambao utakuwa ni wa mzunguko wa pili, utakaopigwa Oktoba 1.

Dodoma Jiji imetoka kushinda bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mtupiaji wa bao hilo alikuwa ni Mkandala mwenyewe aliyepachika bao lake la kwanza kwa msimu wa 2021/22 na kuipa pointi tatu muhimu.

Mkandala amesema:"Tupo tayari kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya Simba na kikubwa ni kuona kwamba tunapata pointi tatu," .

Simba ipo Dodoma imetoka kugawana pointi mojamoja na Biashara United katika mchezo wa mzunguko wa kwanza.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live