Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nyota Azam FC aongezwa Taifa Stars

Tepsie Call Stars.jpeg Tepsie Evans

Tue, 23 Aug 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha Mdenmark, Kim Poulsen amemuongeza kiungo Tepsi Evans wa Azam FC kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kuelekea mchezo wa kufuzu Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) dhidi ya Uganda Jumapili Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Timu hizo zitarudiana Septemba 3 Uwanja wa St. Mary's Kitende mjini Entebbe na mshindi atafuzu Fainali za CHAN ambazo zitafanyika nchini Algeria kuanzia Januari 8 hadi 31.

Tepsie Evans ameinesha kiwango bora tangu kuanza kwa msimu mpya 2022/2023 akifunga mabao mawili katika meci mbili alizocheza mpaka sasa na kutoa pasi moja ya bao.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live