Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ntibazonkiza atupia mbili, Yanga kicheko tu

Singida Pic Data Ntibazonkiza atupia mbili, Yanga kicheko tu

Wed, 16 Dec 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

KIRAKA Saido Ntibazonkiza ameanza vyema katika kikosi cha Yanga baada ya kutupia mabao mawili katika mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Singida UTD uliomalizika wakishinda 3-0 katika uwanja wa Liti.

Katika mchezo huo Saido alionekana kuwa bora zaidi katika umiliki wa mpira na kuwafanya mabeki wa Singida wahahe.

Mchezaji huyo pia alikuwa bora katika kutengeneza nafasi kwa wachezaji wenzake lakini umakini wao katika kumalizia ulionekana kuwa changamoto.

Dakika 22 Saido Ntibazonkiza aliifungia Yanga bao la kwanza baada ya kupokea pasi kwa Farid Mussa na yeye aliuchopu mpira juu ya mabeki wa Singida na kukimbia na mpira kisha akaupiga mpira na kwenda moja kwa moja wavuni.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz