Mon, 11 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Moja kati ya sajili zilizokuwa zinasubiriwa kwa hamu Liverpool, ni ujio wa Nabil Fekiro toka Lyon ghafla jini mkata kamba akapita na kupeperusha dili hilo.
Nabil Fekir mwenyewe anakwambia haelewi ilikuwaje usajili wake ukafeli, sababu majeraha ya goti aliyoyapata 2015-16 yaliyomfanya akakaa nje kwa karibia msimu mzima yalikuwa yameshapona.
Lakini cha kushangaza Liverpool wakawa na hofu ya kumsajili na wakamuacha, Fekir anakwambia hata video ya 'welcome to Liverpool' ilikuwa imesharekodiwa ghafla mambo yakabadilika.
Fekir alitua Real Betis ya La Liga ambako ndiko anakokipiga mpaka sasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live