Kampuni ya utengenezaji wa vifaa vya michezo ya Nike ambayo ilikuwa na Mkataba na Ligi Kuu ya England EPL kwa miaka 25 ya utengenezaji wa mipira ya kuchezea kwa Ligi Kuu England imeshindwa kufikia makubaliano ya kuongeza Mkataba na sasa rasmi wataachama mwishoni mwa msimu 2024/25.
Kampuni ya Nike imedumu EPL kwa miaka 25 wakiwa ndio watengenezaji wa mipira ya Ligi Kuu.
Kufeli kwa dili hilo, mpango mzima sasa upo kwa kampuni ya Puma ambao wanakaribia kuchukua dili hili la utengenezaji mipira baada ya kuweka ofa nono mezani.
Kwa mantiki hiyo Puma atahusika katika Ligi kama;
La Liga
Serie A
Premier League