Unaambiwa Arsenal wamefanya biashara ya hasara kwa aliyekuwa nyota wao Nicolas Pepe, ambapo usajili wa nyota huyo katika klabu ya Arsenal uliweka rekodi ya kuwa mchezaji ghali zaidi kusajiliwa na klabu hiyo mwaka 2019 ambapo aligharimu pauni milioni 72, lakini hivi sasa nyota huyo ameondoka klabuni hapo kwa uhamisho huru.
Pepe hivi sasa yupo Istanbul Uturuki ambapo anatarajiwa kujiunga na klabu ya Trabzonspor akitokea Arsenal. Pepe alifunga mabao 27 katika mechi 112 alizochezea Arsenal, lakini alitumia muda wote wa msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya Nice ya Ligue 1.
Timu gani nyingine unahisi usajili wao wamepigwa kama Arsenal?