Ukweli ni kwamba Mamelod Sundowns ambao wanakwenda kukutana na Yanga katika Hatua ya Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika ni wakubwa kuliko Yanga.
Mamelodi ni wakubwa kuanzia kwenye quality ya wachezaji, uwekezaji, uzoefu wa michuano hii na miundo mbinu…lakini mimi binafsi nimefurahi hawa watu kukutana.
Huwezi kuwa mkubwa kama unaogopa kukutana na wakubwa,umefika muda wa kuipima project ya Yanga maana kila siku tunasema wana timu nzuri,ni muda wa kupima kikosi chao ni muda wa kumpima Gamond,ni muda wa kujua wapi panapwaya.
Hii ni test kubwa kwa Yanga na kama watavuka hapa basi watafika fainali.