Waswahili wanasema "mchawi mpe mtoto akulelee" ndicho walichokifanya Shirikisho la Soka Barani Ulaya(UEFA) mchana huu wakati wa kuchezesha Droo ya hatua ya 16 bora.
Lionel Messi atakua mwenyeji wa Cristiano Ronaldo katika mchezo wa kwanza kabla ya Ronaldo nae kumKaribisha Messi katika mchezo wa marudiano ndani ya Old Trafford, michezo ya hatua ya 16 bora.
PSG watamenyana na Man United katika hatua ya 16 bora michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.
Kwa miaka takribani 10, nyota wawili wa vilabu hivyo wamekua katika viwango vya juu kabisa duniani, na kuleta ubishani mkubwa kwa wapenzi wa wachezaji hao.