Fri, 22 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka Bongo Nasir Khalfan amesema haoni kama mjadala wa kuwafananisha wachezaji wa Al Ahly na Simba SC una afya kwani unaweza kuwanyong'onyeza mashabiki wa Simba.
Amesema uwezo walionao wachezaji wa Al Ahly ni ardhi na mbingu kuwafananisha na wale wa Simba na mchezaji pekee ambaye walau anaweza kupambana na pengine kupata nafasi ya kucheza Al Ahly ni mlinzi wa kati wa Simba,Henock Inonga.
"Walau Inonga anaweza kupambana akapata namba kama akiacha masihala," alisema Nasri.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live