Nyota kutoka klabu ya PSG na timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr (30) hivi sasa yupo mbioni kuvunja rekodi ya gwiji wa mpira wa miguu nchini Brazil, Edson Arantes maarufu kama “Pele”, ambapo anahitaji magoli mawili tu ili kufikia rekodi hiyo ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika timu ya taifa ya Brazil.
Nyota kutoka klabu ya PSG na timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr (30) hivi sasa yupo mbioni kuvunja rekodi ya gwiji wa mpira wa miguu nchini Brazil, Edson Arantes maarufu kama “Pele”, ambapo anahitaji magoli mawili tu ili kufikia rekodi hiyo ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika timu ya taifa ya Brazil. Mpaka hivi sasa Pele ndiye nyota pekee nchini Brazil anayeshikilia rekodi hiyo ya kuwa mfungaji bora wa muda wote katika timu ya taifa ambapo amefunga jumla ya magoli 77 katika michezo 92, ambapo kwa sasa Neymar ameifungia timu hiyo ya taifa mabao 75 hivyo amebakisha magoli 2 tu ili aweze kuvunja rekodi hiyo ikiwa ni mojawapo ya ndoto yake katika maisha ya soka kwenye timu ya taifa ya Brazil.