Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Neymar: Nilijaribu kila Kitu ili kufanikisha kurudi Barcelona

Neymar Jr Santos Neymar Jr

Thu, 24 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshabuliaji wa klabu ya Paris Saint Germain, Neymar amethibitisha kwamba alijaribu kufanya kila kitu awezacho ili kufanikisha uhamisho wake wa kurudi klabu yake ya zamani Barcelona kwenye dirisha la usajiri majira ya kiangazi mwaka 2019.

Mchezaji huyo wa kumataifa kutoka nchini Brazil alihusishwa sana kurudi kwenye klabu yake ya zamani, Neymar alisajiriliwa na klabu ya PSG kwa uhamisho uliovunja rekodi ya Dunia kwenye kipindi cha dirisha la usajiri.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 30 kwa sasa alikuwa na shauku ya kutaka kuunga na mshambuliaji mwenza Lionel Messi, ambaye kwa sasa amesajiriwa na klabu ya PSG, kwenye majira ya kiangazi yaliyopita baada ya klabu ya Barcelona kuwa na matatizo ya kifedha na kuondoka akiwa mchezaji huru.

“Nilijaribu kurudi Barcelona, tulijaribu kila kitu, lakini haikuwezekana, nina furaha Messi amepata nafasi ya kuja PSG, yeye ni rafiki yangu na tunaishi vizuri.”

Neymar amethibitisha kuwa alifanya kadri awezavyo ili kurudi kwenye ligi ya La Liga, ila kwa sasa anafuraha baada ya kuungana na mshindi mara saba wa Ballon d’Or winner.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live