Mabosi wa Newcastle United wamepanga kukubali ofa ya moja wapo ya timu kutoka Saudi Arabia ili kumuuza winga wao wa kimataifa wa Ufaransa, Allan Saint-Maximin, 26, katika dirisha hili.
Mabosi wa Newcastle United wamepanga kukubali ofa ya moja wapo ya timu kutoka Saudi Arabia ili kumuuza winga wao wa kimataifa wa Ufaransa, Allan Saint-Maximin, 26, katika dirisha hili. Vigogo hawa wanataka kumuuza Maximin ili kuongeza pesa itakazozitumia kukamilisha usajili wa winga wa Leicester City ambayo imeshuka daraja msimu uliopita, Harvey Barnes, 25 na inahitajika zaidi ya Pauni 40 milioni ili kuuzwa.