Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Neville: United inavutia sokoni kuliko Liverpool

Nevilleeeeeeeeeeee Garry Neville

Sat, 3 Dec 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Gwiji wa zamani wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya England, Gary Neville anaamini klabu ya Manchester United ni bora zaidi sokoni kuliko klabu ya Liverpool.

Gwiji huyo anaamini klabu ya Man United inavutia sokoni zaidi na inaweza kuzalisha faida ukilinganisha na Liverpool endapo klabu hizo zitanunuliwa kipindi hichi ambacho wamiliki wa vilabu hivo wameviweka sokoni.

Liverpool na Manchester United ambazo zimewekwa sokoni na wamiliki wake huku familia ya Glazer ikitangaza ipo tayari kupokea ofa kwa klabu ya United huku Liverpool wamiliki wake kampuni ya kimarekani ya Fenway Group nao wakitangaza kuiuza klbu hiyo.

Licha ya klabu ya Liverpool kufanya vizuri kwa miaka kumi iliyopita lakini Neville anaamini klabu yake ya zamani itawavutia wawekezaji zaidi sokoni kuinunua kuliko klabu ya Liverpool kwakua United ina uhakika wa kuazalisha faida kuliko vijogoo wa Anfield.

Gary Neville anasema hataki kuidharau klabu ya Liverpool kwakua ni moja ya klabu kubwa zaidi nchini Uingereza lakini ukweli ni kua ukiangalia mapato ya klabu Manchester United inaongoza mbele ya klabu ya Liverpool.

Gwiji huyo ameeleza kua kitu kitakachowaisadia Liverpool ni labda kuwe na tajiri mkubwa sehemu shabiki wa klabu hiyo na muaminifu kwa klabu hiyo lakini kwenye suala la kuvutia wawekezaji Man United bado itakua juu ya Liverpool

Chanzo: www.tanzaniaweb.live