Wed, 21 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha timu ya Taifa ya Burundi Intamba Murugamba, kinatarajiwa kutangazwa Alhamis hii ikiwa ni katika maandalizi ya kuwania kufuzu kombe la Afrika nchini Morocco mwaka ujao.
Chini ya kocha Etienne Ndayiragije Intamba Murugamba itakuwa na kibarua dhidi ya Malawi tarehe 5 Septemba kabla ya kukipiga na Senegal Septemba 9,2024 nchini Malawi.
Kabla ya kukwea pipa kuelekea Malawi timu ya taifa itafanyia mazoezi mkoani Ngozi Agosti 26 katika kujiweka sawa.
Burundi inawania kufuzu ikipambana na nchi za Burkina Faso, Senegal na Malawi katika kundi lake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live