Sat, 18 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Primia Ligi) msimu wa 2021/2022 imeingia hatua ya mzunguko wa tisa na tayari mechi tatu zimeshacheza siku ya Ijumaa Disema 17.
Yanga bado anaendelea kuongoza Ligi mpaka sasa akiwa kileleni na alama zake 20 akifuatiwa kwa karibu kabisa na bingwa mtetezi Simba SC mwenye alama 18 katika nafasi ya pili.
Mtibwa Sugar kutoka Morogoro ndio wanaoburuza mkia katika nafasi ya 16 huku Mbeya kwanza wakiwa nafasi ya 15.
NB: Msimamo huu ni kabla ya mechi za leo Disemba 18, 2021.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live