Sun, 4 Apr 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
TIMU ya Namungo leo inashuka kwenye dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kukwaana na Nkana ya Zambia katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi.
Namungo wanashuka uwanja leo huku wakiwa na rekodi mbaya baada ya kupoteza mechi mbili za awali, hivyo kuwafanya kutokuwa na pointi hata moja.
Hatahivyo, timu hiyo imetamba kuibuka na ushindi dhidi ya timu hiyo ya Zambia, ambayo imekuwa iifanya vizuri katika mechi zake, ili kurejesha matumaini.
Chanzo: www.habarileo.co.tz