Sun, 2 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji wa kusini, Namungo FC wamepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara licha ya sare ya bila kufungana na KMC katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Namungo FC inafikisha pointi 11 katika mchezo wa tano na kupanda juu ya msimamo, ikizizidi pointi moja moja zote Simba na Yanga ambazo hata hivyo zina mechi moja moja mkononi.
Kwa upande wao, KMC wanafikisha pointi sita katika mchezo wa tano pia na kusogea nafasi ya tisa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live