Fri, 24 Nov 2023
Chanzo: Mwanaspoti
Wenyeji, Namungo FC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ihefu SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jana Novemba 23 Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Mabao ya Namungo FC yamefungwa na kiungo Pius Buswita dakika ya 36 na mshambuliaji Hamad Majimengi dakika ya 76.
Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 11 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Ihefu SC inabaki na pointi zake nane nafasi ya 15 kwenye ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi 10.
Chanzo: Mwanaspoti
Related Articles: