Wenyeji wa Kusini, Timu ya Namungo FC wameibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Ihefu SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku wa Jumanne Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
Wenyeji wa Kusini, Timu ya Namungo FC wameibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Ihefu SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara usiku wa Jumanne Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Mabao ya Namungo FC yamefungwa na Seidou Blandja dakika ya 28 na Shiza Kichuya dakika ya 60 na kwa ushindi huo wanafikisha pointi 22 katika mchezo wa 17 na kusogea nafasi ya saba, wakati Ihefu SC inabaki na pointi zake 14 za mechi 17 nafasi ya 14.