Sat, 29 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jana Ijumaa, Julai 28, 2023, jioni umepigwa mchezo wa kirafiki wa maandalizi ya msimu mpya wa 2023/24, kati ya Wauaji wa Kusini, Namungo FC dhidi ya miamba ya Congo DR, AS Vita Club katika dimba la Black Rhino Academy Karatu.
Bao pekee la kiungo Frank Domayo limewapatia The Southern Killers ushindi wa 1-0.
FT: Namungo FCZ1-0 AS Vita.
AS Vita ambao wameweka Kambi ya siku 14 nchini Tanzania kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao, wanatarajia kucheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania, Yanga Sc hivi karibuni.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live