Tue, 21 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa Timu ya Taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars, Michael Olunga ameachwa nje ya kikosi kitakachoshiriki mechi za kufuzu Kombe La Dunia mwezi ujao dhidi ya mabingwa wa AFCON Ivory Coast na Burundi.
Hii ni baada ya kocha wa Kenya Engin Firat kutaja kikosi chake cha awali Jumatatu.
Ingawa Eric ‘Marcelo’ Ouma, Joseph Okumu, na Jonah Ayunga wameachwa nje kutokana na majeraha, sababu za kuachwa nje kwa Olunga hazijabainika kufikia sasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live