Thu, 15 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nahodha wa timu ya Taifa ya Ivory Coast Max Gradel (36) alitoa heshima kwa marehemu Cheick Tioté wakati wa gwaride lao la ubingwa wa kombe la AFCON 2023 siku ya Jumatatu.
Tioté alifariki Juni 5, 2017 huko Beijing, China baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo akiwa mazoezini.
Wawili hao walikuwa sehemu ya kikosi cha Ivory Coast kilichotwaa ubingwa wa AFCON 2015.
Kama angekuwepo, Tioté angekuwa na umri wa miaka 37.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live