Wed, 15 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ni kama tayari amekwishauaga msimu wa 2021/2022. Ndivyo unavyoweza kusema kwa kiungo hatari wa Azam FC iddi Nado ambae majeraha aliyoyapata yatamuweka nje kwa muda wa miezi tisa.
Taarifa hiyo imetolewa na Azam FC, baada ya kupata majibu ya uhakika kutoka kwa wataalamu na sasa Nado yuko nchini Afrika ya Kusini akipatiwa matibabu.
Nado aliumia katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar Novemba 30 katika mchezo walioibuka na ushindi wa bao 1-0.
Sikiliza kilichosemwa na Azam FC
Chanzo: www.tanzaniaweb.live