Klabu ya Far Rabat ya nchini Morocco, anayofundisha kocha Nasreddine Nabi wametuma ofa kulizia uwezekano wa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Klabu ya Yanga, Stephanie Azizi KI.
Taarifa kutoka nchini Morocco zineleza kuwa, AS FAR wameweka kiasi dola za Kimarekani 700,000 (sawa na Tsh bilioni 1.82) kama ada ya usajili kwa nyota huyo wa Burkna Faso.
Hata ivyo ofa yao uenda ikatupiliwa mbali kutokana na uwepo wa vilabu vingi vikubwa vilivyo onyesha uhitaji wa mchezaji huyo huku Yanga nao wakijipapatua kumbakisha top-scorer huyo wa NBC-PL mpaka sasa.
Mbali na hilo, Azizi K alionekana kuwahidi mashabiki wa Yanga kuwa anapendelea kusalia ndani ya Yanga kwani malengo yake ya kufika fainali ya CAFCL na kubeba ubingwa akiwa na Yanga bado hayajatimia, hivyo anauachia uongozi wa Yanga kukamilisha taratibu ili yeye aweze kusaini mkataba mpya.