Kocha wa Yanga, Nasredinne Nabi amewapumzisha mastaa wanne walioanza kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho barani Afrika walioshinda kwa bao 1-0 ugenini dhidi ya Club Africain ya Tunisia.
Yanga itavaana na Kagera Sugar muda mfupi ujao katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza kwenye mchezo wa Ligi Kuu utakaoanza saa 10:00 jioni.
Mastaa waliopumzishwa leo ambao walianza dhidi ya Club Africain ni Bernad Morrison, Jesus Moloko, Khalid Aucho na Yanick Bangala huku Kocha Nabi akiifungia kazi Kagera Sugar akianza na mabeki wa kati watatu na washambuliaji wawili.
Nabi ameingia na mfumo wa 3-5-2 ambapo langoni ameanza na kipa, Djigui Diarra, mabeki wa pembeni Kibwana Shomari na Joyce Lomalisa huku mabeki watatu wa kati wakiwa ni Bakari Mwamnyeto, Dickson Job na Ibrahim Bacca.
Viungo ni Zawadi Mauya, Salum Abubakar 'Sureboy' na Feisal Salum 'Feitoto' huku washambuliaji wakiwa ni Fiston Mayele na kinda Clement Msize.
Wachezaji wa akiba ni; Abuutwalib Mshery, Yanick Bangala, Djuma Shaban, Khalid Aucho, Jesus Moloko, Bernad Morrison, Yusuph Athuman, Farid Mussa na Tuisila Kisinda.