Kocha Mkuu wa Kaizer Chiefs, Nasreddine Nabi amesema kuwa vilabu vya nchini Afrika Kusini vimekuwa vikikataa kuwauzia wachezaji timu hiyo.
nabi ambaye amewahi kuifundisha Yanga SC kwa mafanikio makubwa amesema kuwa huenda huo ni mpango mkatati wa vilabu vya Afrika Kusini kuidhoofisha Kaizer.
"Vilabu vingi vya Afrika kusini havitaki kuuza wachezaji kwa Kaizer Chiefs sielewi kwanini?wako tayari kuuza wachezaji kwa vilabu vingine vya hapa lakini sio kwetu sisi Kaizer Chiefs.
"Labda ni mbinu au chuki dhidi yetu lakini ni ngumu mno kusajili wachezaji kutoka katika vilabu vya hapa ligi kuu Afrika Kusini," amesema Nabi.