Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Limetangaza viingilio vya mchezo wa Ngao ya Jamii kuelekea ufunguzi wa msimu mpya 2022/2022.
Mchezo huo unavikutanisha vilabu vikongwe nchini na wapinzani wa Jadi Simba na Yanga.
Mchezo huo wa Ngao ya Jamii utapigwa Agosti 13 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kumbu kumbu zinaonesha mchezo huo kwa mwaka uliopita uliwakutanisha watani hao na Yanga wakaibuka kinara kwa bao la pekee lililowekwa wavuni na Fiston Mayele.
Viingilio katika mchezo huo, ni vya aina tano ambavyo ni kama vifuatavyo;
VIP A- 30,000
VIP B- 20,000
VIP C- 15,000
Viti vya Rangi Machungwa - 7000
Viti vya Bluu & Viti vya Kijani - 5000