Sun, 13 Aug 2023
Chanzo: Tanzania
Hayawi hayawi, hatimae yamekuwa. Dabi ya Kariakoo ndani ya Dimba la Mkwakwani Jijini Tanga inakwenda kuanza muda mchache kutoka sasa.
Ni Fainali ya Ngao ya Jamii 2023, ambapo wanakutana watani wa Jadi Simba na Yanga katika mcheozo ulioteka hisia za wengi.
Kila timu imetamba kumtandika mwenzake kutokana na ubora wa kikosi ilichonacho lakini dakika ndizo zitakazoamua mbabe.
Wakati Simba wakipata pengo kwa mlinzi wao Henock Inonga, Yanga wanamkosa winga wao Skudu Makudubela
Hivi hapa vikosi vya timu zote mbili vinavyoanza mchezo wa leo
Chanzo: Tanzania