Mchezo wa kumsaka mshindi wa tatu Ngao ya Jamii 2023 unapigwa majira ya saa tisa Alasiri katika Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Mchezo huo unawakutanisha matajiri wa Jiji la Dar es Salaam Azam FC dhidi ya walima alizeti wa Singida FG.
Azam wameangukia hatua hiyo baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Yanga huku Singida wakipigwa kwa changamoto ya mikwaju ya penati kutoka kwa Simba SC.
Timu zote zinataka kupata ushindi katika mchezo wa leo angalau kuwapa furaha mashabiki wake hasa baada ya sajili kubwa zilizofanywa na timu hizo.
Hivi hapa vikosi vya timu zote mbili vinavyoanza mchezo wa leo;