Thu, 18 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nusu fainali za michuano ya Ngao ya Jamii ikiwa ni ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu mpya 2024/2025 zitapigwa Agosti 8 Dar es Salaam na Zanzibar.
Yanga na Simba zitakutana katika nusu ya pili kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam wakati Azam itavaana na Coastal Union katika nusu ya kwanza kwenye uwanja wa New Amaan, Zanzibar.
Mchezo wa kusaka mshindi wa tatu utatangulia Agosti 11 kabla ya fainali kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam.
Ligi Kuu Tanzania Bara imepangwa kuanza Agosti 16.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live