Wed, 8 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Licha ya Coastal Union kushikilia bomba vya kutosha lakini ukubwa wa wachezaji wa Yanga SC umeamua matokeo kwa Yanga kushinda 1-0.
Mechi imepigwa leo Novemba 8, 2023 kwenye uwanja wa CCM Mkwakani jijini Tanga.
Goli la Yanga liliwekwa kambani na Clement Mzize ambaye aliingia kipindi cha pili na kubadili matokeo akichukua nafasi ya Kennedy Musonda.
Yanga wamezidi kujikita kileleni wakiwa na alama 24 wakicheza michezo 9 ya Ligi Kuu ya NBC huku Coastal Union wakiwa nafasi ya 13 na alama zao 7.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live