Fri, 19 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchezo wa Ligi Kuu unaoendelea katika Uwanja CCM kirumba Jijini Mwanza umezalisha magoli matatu katika dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Ni Simba walio chini Mhispania Pablo Franco Martin wanaongoza kwa magoli matatu yaliyofungwa na Meddie Kagere dakika ya 17' na 37'.
Goli la tatu la Simba limefungwa na Kibu Dennis ambae anaifungia klabu yake mpya goli la kwanza msimu huu, akimalizia pasi safi ya Shomari Kapombe.
Simba wamekwenda mapumziko wakiwa kifua mbele kwa idadi ya magoli 3-0.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live