Vigogo wa Kariakoo Simba na Yanga wanahesabu dakika tu kuja kupimana ubavu mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara katika Dimba la Benjamin Mkapa.
Mchezo huo unaovuta hisia za wengi unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa hasa ikizingatiwa timu hizo zinalingana alama wote wakiwa na alama 18 Yanga wakikamata nafasi ya pili na Simba wakikamata nafasi ya tatu.
Ushindi katika mchezo wa leo utamfanya mshindi kwenda kuongoza jedwali la msimamo wa Ligi ambalo kwa sasa Azam ndio kinara wakiwa na alama zao 19.
Yanga watahitaji kulipa kisasi baada ya kupoteza mchezo wao wa mwisho walipokutana kwenye Ligi baada ya kukubali kichapo cha magoli 2-0, magoli ya Inonga Baka na Kibu Denis.
Hivi hapa vikosi vya Timu zote mbili vinavyoanza mchezo wa leo;
Simba SC:
Manula
Kapombe
Zimbwe Jr
Che Malone
Inonga
Kanoute
Ngoma
Chama
Kibu D
Saido
Baleke
Yanga SC:
Diarra
Yao
Lomalisa
Bacca
Job
Aucho
Mudathir
Maxi
Pacome
Aziz Ki
Musonda