Wed, 14 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC wapo kule Jijini Mbeya kuwakabili maafande wa Magereza timu ya Tanzania Prison kutoka Jijini Mbeya, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Simba wana kila sababu ya kusaka ushindi katika mchezo huo hasa katika nyakati hizi ambazo anapambana ili kurejesha Ubingwa alioupoteza kwa Yanga msimu uliopita.
Simba wamekuwa na mchezo mgumu wanapokutana na Prisons lakini watahitaji ushindi ili kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi.
Hiki hapa Kikosi cha Simba kinachoanza mchezo wa leo;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live