Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wanashuka dimbani muda mchache ujao kuwakaribisha wakusanya ushuru wa Manispaa ya Kinondoni timu ya KMC.
Mchezo huo unachezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa huku Kocha Matola akiwa na jukumu la kukisimamia kikosi hicho baada ya kuachana na Kocha wao Zoran Maki alietimkia nchini Misri.
Mchezo huo wa mzunguko wa tatu unatazamwa kwa macho mawili na Simba katika kuzisaka pointi tatu ili kujikita kileleni baada ya jana watani wao kulazimishwa sare.
Simba imeshacheza michezo miwili na kujikusanyia alama 6 hivyo ushindi wa leo utawapeleka kileleni mwa msimamo wa Ligi kwa kujikusanyia alama 9.