Sat, 13 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bra, Timu ya Yanga wanahitaji alama tatu tu kutangazwa kuwa Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2022/2023.
Yanga watakuwa nyumbani jioni ya leo kuwakaribisha Timu ya Dodoma Jiji Mchezo utakaopigwa katika Uwanja wa Chamazi Complex.
Yanga wanahitaji kushinda mchezo huo ili kupata wasaa mzuri wa kujiandaa na mchezo wa mkondo wa pili wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Marumo Gallanys ya Afrika ya Kusini.
Hiki ndicho kikosi cha Yanga kinachoanza mchezo wa leo muhimu katika mbio za kusaka taji la Ligi Kuu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live