Sun, 10 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC wanashuka Dimbani muda mchache kutoka sasa kuvaana na Polisi Tanzania.
Mchezo huo utapigwa katika Uwanja wa Ushirika, Moshi huku Simba wakihitaji alama tatu ili kupunguza wigo wa alama baina yake na Yanga.
Mpaka sasa Simba anazidiwa alama 11 na Yanga, hivyo ushindi katika mchezo wa leo utawafanya kuwa na tofauti ya alama 8 pekee.
Hiki hapa kikosi cha Simba kinachoanza mchezo wa leo;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live