Tue, 13 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za kipindi cha kwanza zinakamilika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar.
Yanga wanakwenda mapumziko wakiwa na uongozi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar kutoka Morogoro.
Yanga wametengeneza nafasi nyingi ambazo pengine wangekuwa makini wangekuwa na idadi kubwa ya magoli mpaka sasa.
Mchezo huu umekuwa na matumizi makubwa ya nguvu, huku Ilanfya wa Mtibwa Sugar akicheza madhambi mara kwa mara.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live