Sun, 30 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za kipindi cha Kwanza zinakamilika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba dhidi ya Mtibwa Sugar kutokea Mkoani Morogoro.
Simba wanakwenda mapumziko wakiwa kifua mbele kwa uongozi wa goli 1-0 lililofungwa na kiungo Mzamiru Yassin dakika ya 38 akimaliza pasi safi kutoka kwa Augustine Okrah.
Mtibwa wanalazimika kucheza pungufu baada ya mchezaji wao Pascal Kitenge kuoneshwa kadi nyekundu kwa mchezo usio wa kiungwana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live