Sat, 23 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za Kipindi cha Kwanza zinakamilika katika Dimba la Benjamin Mkapa huku zikiacha burudani safi kwa wapenzi wa Kandanda.
Yanga wanakwenda mapumziko kifua mbele wakiwa na uongozi wa magoli 2-1, yaliyowekwa kambani na Fiston Mayele na Feisal Salum, huku lile la Namungo likifungwa na Shiza Kichuya.
Rekodi ya Timu hizi ndio inayowafikirisha mashabiki huku kukiwa hakuna timu iliyowahi kufanikiwa kumfunga mwenzake.
Pengine kipindi cha pili tutaona walimu wakijaribu kubadilisha mbinu ili kuhakikisha wanaondoka na alama tatu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live