Sun, 30 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mambo yanazidi kutakata kwa Wekundu wa Msimbazi, Simba mbele ya wageni Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Augustine Okrah na Moses Phiri wanaipa Simba uongozi wa magoli 4-0 huku kwa mara nyingine Mtibwa Sugar wakishuhudia kadi nyekundu ya pili kwa upande wao.
Cassian Ponera anaoneshwa kadi nyekundu na kuwafanya Mtibwa kucheza wachezaji nane Uwanjani huku mlinda mlango akiwa mtu wa 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live