Wed, 7 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mambo yanakwenda mrama kwa Simba SC ndani ya dakika 60 za mchezo tayari wameahakubali kuwa nyuma kwa magoli 2-1 dhidi ya KMC.
George Makang’a dakika ya 57 anaiandikia KMC bao la pili maridadi akimuacha Aishi Manula analalama na walinzi wake.
Simba katika jitihada za kutaka kusawazisha wanafanya mabadiliko kwa kumuingiza Mzamiru Yassin na John Bocco wakichukua nafasi za Nassoro Kapama na Okrah.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live