Wed, 7 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji raia wa Zambia Moses Phiri ndani ya dakika 2 tangu mwamuzi Ramadhan Kayoko kupuliza kipyenga cha kuashiria kuanza kwa mchezo anaiandikia Simba bao la uongozi.
Phiri aliwahadaa walinzi kadhaa wa KMC kabla ya kuachia shuti kali lililotinga wavuni na kumuacha mlinda mlango wa KMC asijue la kufanya.
Simba wameanza mchezo wa leo kwa kasi na yote ni katika kuhakikisha wanaondoka na alama tatu katika mchezo huu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live