Wed, 3 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bado hakuna alieweza kuliona lango la mwenzake ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza katika dimba la Mkapa Dar es Salaam, ambapo Simba wamewakaribisha Namungo FC.
Mchezo umetawaliwa na matumizi makubwa ya nguvu huku Simba wakitawala eneo kubwa la mchezo.
Simba wamekosa nafasi kadhaa za wazi ambazo pengine kama wangezitumia vyema labda wangekua mbele kwa magoli mawili.
Bernard Morisson muda mwingi amekuwa akiwasumbua mabeki wa namungo na anaonekana kuwa tishio.
Bila shaka kipindi cha pili walimu watakuja na mbinu mbadala kuhakikisha wanaibuka na ushindi kila upande.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live