Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mzize apitishwa njia za staa wa Man United 'Chicharito'

Mzize Msk21 Mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize

Sat, 13 Apr 2024 Chanzo: Mwanaspoti

Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Francis Baraza amempa mbinu mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize za kumfanya awe mshambuliaji bora Afrika.

Akizungumza Baraza amesema Mzize ni mchezaji mzuri na mkubwa kama atafanyia kazi mambo kadhaa na "sioni akicheza Tanzania, ni mchezaji mzuri."

"Kwanza anatakiwa kufanyia kazi suala la umaliziaji, namshauri aangalie video za mchezaji wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez 'Chicharito' na kujaribu kufanya mazoezi ya kufunga akiwa mwenyewe bila kipa golini,"

"Mzize ni mshambuliaji mzuri aache kukokota sana mipira, anafanya hivyo kwasababu ana nguvu na uwezo wa kusumbua mabeki, shida ni moja tu kwenye kumalizia... ukiangalia kwa washambuliaji waliopo msimu huu yeye ni mchezaji ambaye anatengeneza nafasi nyingi," alisema na kuongeza

Hakuna mshambuliaji ambaye anatengeneza nafasi nyingi za kufunga kama Mzize akiwa ndani ya boksi shida ni kukosa umakini wa umaliziaji akiongeza walio na ubora zaidi katika kumalizia, wanapambana sana ili kupata nafasi kama anazopata.

Amesema ili Mzize aweze kuwa bora anatakiwa kukaa kwenye maeneo na kutumia nafasi bila kutafuta ushindani na mabeki ndani ya 18 huku akikiri kuwa endapo atafanyia kazi mambo hayo anamuona akiondoka Tanzania.

"Mzize akifanyia kazi hayo mambo niliyoyasema hapo sioni akicheza soka la Tanzania na mimi nipo upande wake siku zote, nampongeza kocha Miguel Gamondi kwa kuendelea kuamini katika kipaji hicho kwa kumpa nafasi," alisema na kuongeza;

"Licha ya mashabiki kumzomea kutokana na kukosa nafasi lakini kocha Gamondi amewapa kisogo ameendelea kumpa nafasi na anafanya vizuri juzi katuadhibu kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho ameukokota mpira katikati ya mabeki na kufunga ni mchezaji mwenye nguvu na anajiamini," alisema.

AIPA YANGA UBINGWA

Wakati huo huo, Baraza alisema Yanga wana timu ambayo imekamilika kila eneo huku akitaja mchezaji mmoja kila nafasi kuwa wana kila sababu ya kuipa ubingwa timu.

"Tumekutana na Yanga kwenye mechi za ligi na FA zote tumepoteza licha ya kucheza mchezo mzuri dhidi yao, sababu kubwa ni kutokana na namna walivyo na wachezaji wazuri na wazoefu," alisema na kuongeza;

"Yanga wana Djigui Diarra golini ni kipa mzuri na mzoefu, Ibrahim Abdallah 'Bacca' beki mzuri, Khalid Aucho na Jonas Mkude eneo la kiungo wote ni wazoefu na wanaipambania timu kuhakikisha inapata matokeo," alisema na kuongeza;

"Ukiachana na eneo hilo ambalo kwa kiasi kikubwa limefanya kazi nzuri kumlinda Diarra pia wana Stephane Aziz Ki, Pacome Zouzoua na Mzize ambaye licha ya uchanga wake lakini anakomazwa na ubora wa wachezaji anaocheza nao," alisema.

Baraza alisema Yanga imekamilika sana na Gamondi hana kazi kubwa ya kuwafundisha wachezaji wake zaidi ya kuwajenga kimbinu na kuwaweka pamoja ili wacheze kwa kushirikiana kwasababu tayari kila mchezaji ni mkomavu na ana uchu wa mafanikio.

"Wameshajijenga kitimu na ndio maana tunashuhudia kuna timu zinafungwa mabao 5-0 na zisipoangalia na kujiimarisha zaidi kuna timu zitafungwa mabao saba kwani muunganiko wa timu hiyo sioni watu wa kuwazuia kutwaa taji la msimu huu," alisema.

Chanzo: Mwanaspoti
Related Articles: