Mon, 19 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muda wa kukua umeisha kwa Clement Mzize... Kwa sasa anatakiwa kujifunza akiwa kazini 'On The Job Training'...
Maana yake makosa yapungue kulingana na anavyoaminiwa na presha iliopo pale mbele... Wakati yupo Mayele watu waliuelewa na kuukubali uhitaji wa yeye kukua lakini kwa sasa anatakiwa kuhesabika kikamilifu maana kwa hali inayoendelea anaweza kabisa kuendelea kuwa mshambuliaji namba moja kwenye kikosi na anatakiwa kutimiza ukubwa wa jukumu hilo...
Kwa uchache alitakiwa kuondoka na magoli mawili katika mchezo dhidi ya Prisons kama sio hata Hattrick...
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: