Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka East Africa Radio, Samwel Rashid mwenyewe anajiita Wakanda Republic amesema kuwa, eneo ambalo Simba wanapaswa kuliboresha ni kiungo mkabaji.
Wakanda amesema kuwa makocha ambao wamepita Simba hivi karibuni walikuwa wakimtumia Sadio Kanoute kama kiungo mkabaji lakini kiasili sio nafasi yake.
Simba tayari wameshamsajili kiungo mkabaji, Babacar Sarr raia wa Senegal kama mchezaji huru akitokea US Monastir ya Tunisia baada ya kumaliza mkataba wake.
"Simba hivi sasa eneo ambalo mimi naona ni muhimu sana na ambalo wanahitaji kulifanyia maboresho ni eneo la kiungo mkabaji. Hii position ndiyo imewahukumu Simba kwenye michezo mingi sana, ni eneo ambalo Robertinho ame-struggle sana akijaribu ku-switch wachezaji lakini haikuonekana kupata suluhisho.
"Sasa hivi amekuja Benchikha ambaye angalu sasa hivi tunamuona anamtumia Sadio Kanoute pamoja na Fabrice Ngoma, lakini kiungo mkabaji wake ambaye ni Primary ni Sadio Kanoute, muda ambao anakosekana Kanoute akiingia Mzamiru, Mzamiru hakupi kile ambacho Kanoute huwa anakupa," amesema Wakanda Republic.
Wachezaji wa Kigeni Simba mpaka sasa ni 13 hivyo wanatakiwa kupunguza mchezi mmoja wa kimataifa ili kukidhi kanuni;
Willy Onana
Moses Phiri
Clatous Chama
Luis Miquissone
Sadio Kanoute
Fabrice Ngoma
Ayoub Lakred
Henock Inonga
Che Malone
Jean Baleke
Aubin Kramo
Saido Ntibazonkiza
Babacar Sarr - Usajili mpya.