Kocha Mkuu wa Klabu ya Namungo FC ambaye ni Raia wa DR Congo Mwinyi Zahera amesema Taifa Stars haiwezi kuifunga Congo katika mchezo wa leo kuwania kufuzu kuingia 16 bora katika fainali za mataifa ya Afrika AFCON 2023 yanayoendelea nchini Ivory Coast.
Kocha Mkuu wa Klabu ya Namungo FC ambaye ni Raia wa DR Congo Mwinyi Zahera amesema Taifa Stars haiwezi kuifunga Congo katika mchezo wa leo kuwania kufuzu kuingia 16 bora katika fainali za mataifa ya Afrika AFCON 2023 yanayoendelea nchini Ivory Coast. Taifa Stars inashuka dimbani kucheza dhidi ya DR Congo saa 5:00 usiku uwanja wa Amadou Gon Coulibaly na team yoyote itakayoshinda inafuzu hatua ya 16 bora.