Thu, 29 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa daktari wa Azam Fc Mwanandi Mwankemwa atazikwa leo saa 10 jioni katika makaburi ya Kinondoni.
Mwili wa marehemu utaswaliwa msikiti wa Bakwata Kinondoni kabla ya kwenda kuzikwa.
Kwa sasa msiba upo nyumbani kwake Mwanagati.
Dk Mwankemwa alifariki dunia Februari 27, 2024 katika hospitali ya Temeke alipokuwa akipatiwa matibabu
Pumzika kwa amani Dk Mwankemwa
Chanzo: www.tanzaniaweb.live